Rais Kagame amempokea Waziri wa Mambo ya Nje wa Tanzania.
Rais Kagame amempokea ofisini kwake Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wa Tanzania, Mahamoud Thabit Kombo. Mazungumzo yao yalilenga kuimarisha zaidi uhusiano mzuri uliopo kati ya Rwanda na Tanzania.


