Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan ametoa Tsh. Milioni 100 ili zikamilishe Ujenzi wa Makumbusho ya Hayati Dkt. John Pombe Magufuli yaliyopo Chato Mkoani Geita.
Makamu wa Rais wa Tanzania, Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi amesema hayo leo March 17,2026 wakati akiongea kwenye Kumbukumbu ya Miaka Mitano ya Hayati Dkt. Magufuli.
“Kwa kutambua na kuenzi mchango wa Hayati John Pombe Magufuli, Rais Samia Suluhu Hassan amekuwa akifuatilia kwa karibu Ujenzi wa Makumbusho yake hapa Chato

Mh. Rais ametaarifiwa kwamba ili Uenzi wa Makumbusho ya Hayati Magufuli ukamilike zimepungua Tsh. milioni 100, nafurahi kuwajulisha kuwa Mh. Rais ameamua kutoa fedha hizo zote ili kukamilisha kazi hiyo”
Bagabo John
