Timu ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars imetupwa nje ya michuano ya Kombe la Mataifa Afrika AFCON 2025 kufuatia kipigo cha 1-0 dhidi ya wenyeji , Morocco katika dimba la Prince Moulay Abdellah mjini Rabat kwenye mchezo wa hatua ya 16 bora.
Morocco imetangulia robo fainali kumsubiri mshindi kati ya Afrika Kusini dhidi ya Cameroon watakaochuana kwenye mchezo mwingine wa hatua ya 16 bora.

