Waziri wa Usalama wa Ndani, Dkt. Vincent Biruta, amewapongeza wafanyakazi wa Jeshi la Magereza nchini Rwanda (RCS) kwa hatua waliopiga katika kuimarisha usawa wa kijinsia na ushirikiano wa kijinsia kazini
Dkt Birutakuwa amesema kuwa Serikali imejipanga kuongeza uwiano wa wanawake ndani ya RCS kutoka asilimia 28.5 ya sasa hadi kufikia asilimia 30.

Aliyasema hayo hii leo Alhamis 28 August 2025 wakati wa uzinduzi rasmi wa Kongamano la 6 la Wanawake Wanaofanya Kazi ya Urekebishaji, lenye kaulimbiu isemayo: “Kujithamini katika Dunia ya Teknolojia: Kukuza Utaalamu na Kuthibitisha Usawa wa Kijinsia.”
Aidha, Waziri Biruta amesisitiza kuwa mkutano huo ni wa muhimu kwa kuwa unachangia katika kuboresha utendaji kazi na ufanisi wa taasisi hiyo.
Bagabo John
