Mtafiti na mwandishi wa vitabu, Hategekimana Richard, amesema kuwa anandaa kuchapisha kitabu alichokiandika kuhusu uchaguzi wa Rwanda tangu enzi za kifalme hadi ule wa hivi karibuni wa Julai 2024, kwa lengo la kuuonyesha ulimwengu utofauti wake ili waweze kujifunza kutokana na uchaguzi huo wanapojiandaa
Richard ambaye ni mwandishi wa vitabu, ametangaza kuwa ameamua kuandika kitabu hiki ili kuepuka historia ya uchaguzi wa Rwanda isije ikaandikwa kinyume na watu wengine kwa sababu huwa wanasema wanavyotaka.
Hategekimana ametangaza kuwa alichambua uchaguzi wa Rwanda kwa kuzingatia nyaraka mbalimbali za mashirika yasiyo ya kiserikali, makundi ya kisiasa na kidini na kugundua kuwa uchaguzi huo ulikuwa kama harusi.


Rais Paul Kagame wakati akipiga kura
Alisema, “Kuandika kitabu hiki ni silaha dhidi ya wale wanaoamini kuwa wanaandika uongo kuhusu mambo mazuri ya Rwanda kwa sababu siku zote wanasema unapotaka kuwaficha Wanyarwanda, uwafiche kwenye vitabu."
Nimeamua kupambana kwamba hakutakuwa na Wageni watakaopotosha historia ya uchaguzi wa Rwanda. Sisi ni nguvu za Rwanda ambayo lazima tuijenge, tukiongozwa na Rais wa Jamhuri Paul Kagame, ambaye tunampenda, anayeunga mkono utawala bora na demokrasia."
Katika kitabu hiki, anaeleza jinsi wafalme wa Rwanda waliishi na jinsi machifu walivyokuwa wa kiteuliwa. Wakati wazungu walipo fika Rwanda waribadilisha kila kitu, katika jamhuri ya kwanza, walikuwa wakitoa mgomba mmoja tuu nahata Jamhuri ya Pili ilikwa hivyo
Hategekimana amesema, “Uchaguzi wa Jamhuri ya kwanza na ya pili ulitokana na dhulma, wananchi sio walioshiriki, lakini chaguzi za kuanzia mwaka 2003 hadi 2024 ni za kidemokrasia, wananchi wana uhuru, wanapiga kura wapendavyo, vyama vingi vya kisiasa na wanashiriki kutoa wagombea

Dr Frank Habineza wakati akipiga kura

Mpayimana Philippe wakati akipiga kura

Hategekimana Richard
Richard Alisema uchaguzi katika nchi mbalimbali una sifa ya vipindi vya machafuko na kusababisha vita kwa namna ambayo maisha ya watu yanapotea, hivyo wanapaswa kujifunza kutokana na uchaguzi wa Rwanda.
Imepangwa kuwa kitabu cha 'Njia ya Rwanda kwenye Kura: Uchaguzi katika Kuzaliwa Upya kwa Taifa' nilichoandika kitatolewa Machi 27, 2025 huko Rusororo kwenye Ukumbi wa Intare katika hafla itakayohudhuriwa na watu elfu tatu.

Kitabu hiki kimeandikwa kwa Kiingereza lakini mwandishi anapanga kukichapisha kwa Kinyarwanda, Kifaransa na Kiswahili.
Bagabo John
