Imam Mohammad Tawhidi, anayejulikana kama "Imam wa Amani" na kiongozi wa Baraza la Maimamu Duniani (Global Imams Council), amewatakia Wakristo wote wanaoadhimisha Krismasi heri njema kupitia ujumbe wake kwenye mtandao wa X
Ujumbe huo umepokelewa kwa njia tofauti na wafuasi wake. Baadhi ya watumiaji wamempongeza kwa kukuza maelewano baina ya dini, huku wengine wakimshukuru kwa msimamo wake wa amani na kuungana na Wakristo, Wayahudi na Waislamu wenye msimamo wa wastani dhidi ya itikadi kali.

Bagabo John
