•     

Ruto Aitisha Mkutano wa Baraza la Usalama la Kitaifa Kufuatia Kifo cha Kiongozi wa ODM

Kwa mujibu wa Ikulu, kikao hicho kilipangwa kufanyika saa 10:30 asubuhi, na kufuatiwa na kikao maalum cha Baraza la Mawaziri saa 2:30 usiku.

Ruto Aitisha Mkutano wa Baraza la Usalama la Kitaifa Kufuatia Kifo cha Kiongozi wa ODM
Ruto Aitisha Mkutano wa Baraza la Usalama la Kitaifa Kufuatia Kifo cha Kiongozi wa ODM

Baraza la Usalama la Kitaifa (BMT) la Kenya ndilo mamlaka ya juu zaidi kuhusu usalama wa taifa, yenye jukumu la kusimamia vyombo vya usalama na kuunganisha sera za ndani, za kigeni na za kijeshi.

Wakiongozwa na rais, wajumbe wa Baraza hilo ni pamoja na Naibu Rais, Makatibu wa Baraza la Mawaziri husika, Mwanasheria Mkuu, Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi ya Kenya, Mkurugenzi Mkuu wa Huduma ya Kitaifa ya Ujasusi, na Inspekta-Jenerali wa Huduma ya Kitaifa ya Polisi. 

Majukumu yake ni pamoja na kutathmini uwezo wa usalama wa taifa, kupeleka vikosi vya kitaifa, na kuripoti kila mwaka kwa Bunge 

Mikutano hiyo ni sehemu ya mashauriano rasmi ya serikali kuhusu mipango ya maombolezo ya kitaifa, ikizingatiwa wadhifa alioshikilia Raila katika anga za kisiasa nchini.

Ruto Aitisha Mkutano wa Baraza la Usalama la Kitaifa Kufuatia Kifo cha Kiongozi wa ODM

Ruto Aitisha Mkutano wa Baraza la Usalama la Kitaifa Kufuatia Kifo cha Kiongozi wa ODM
Ruto Aitisha Mkutano wa Baraza la Usalama la Kitaifa Kufuatia Kifo cha Kiongozi wa ODM

Kwa mujibu wa Ikulu, kikao hicho kilipangwa kufanyika saa 10:30 asubuhi, na kufuatiwa na kikao maalum cha Baraza la Mawaziri saa 2:30 usiku.

Baraza la Usalama la Kitaifa (BMT) la Kenya ndilo mamlaka ya juu zaidi kuhusu usalama wa taifa, yenye jukumu la kusimamia vyombo vya usalama na kuunganisha sera za ndani, za kigeni na za kijeshi.

Wakiongozwa na rais, wajumbe wa Baraza hilo ni pamoja na Naibu Rais, Makatibu wa Baraza la Mawaziri husika, Mwanasheria Mkuu, Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi ya Kenya, Mkurugenzi Mkuu wa Huduma ya Kitaifa ya Ujasusi, na Inspekta-Jenerali wa Huduma ya Kitaifa ya Polisi. 

Majukumu yake ni pamoja na kutathmini uwezo wa usalama wa taifa, kupeleka vikosi vya kitaifa, na kuripoti kila mwaka kwa Bunge 

Mikutano hiyo ni sehemu ya mashauriano rasmi ya serikali kuhusu mipango ya maombolezo ya kitaifa, ikizingatiwa wadhifa alioshikilia Raila katika anga za kisiasa nchini.